Habari Mpya

Thursday, February 13, 2014

NJIA RAHISI YA KUMTAMBUA MTU MGOMVI KWA NJIA YA KISAIKOLOJIA



Wandugu leo hii naomba tuzungumzie jambo moja la kuweza kumtambua mtu aliyegombana na mwenzake kwa kupitia  mawasiliano yao….

Siku zote palipo na upendo utajua tu kwa kuangalia au kusikia namna ya maongezi yao wanavyowasiliana, huwa ni kwa upole na tabasamu lenye kudhihirika waziwazi, tena usipokuwa makini hauwezi kusikia wameongea nini….. ukiona hivyo ujue upendo umetawala kwa kila mmoja au kwa mmoja wao kati ya hao waongeao.

Lakini sasa, Siku zote huwezikuta waliogombana wakiongea kwa upole, na kwa sauti ya chini… mara nyingi wengi wao hujikuta wanaongea kwa kupayuka tena kwa sauti kubwa, na  haijalishi wapo umbali kihasi gani au karibu kihasi cha kugusana.

Kwa udhirisho huo ndiyomaana  nawezakusema unaporuhusu ugomvi kuzidi kuwa mkubwa  kwako, ni dhahiri kabisa ndivyo umbali wa kisaikolojia unavyozidi kuongezeka kati yako na uliyegombana naye,  pasipo wewe mwenyewe kuuona huo umbali, na hautokuja kuuona huo umbali mpaka utakaporuhusu element za upendo ndani yako… nipo taratiiiibu utajikuta unaanza kupunguza umbali uliopo kati yake na Yule au wake aliyogombana nao.

Embu kuanzia sasahivi jiangalie katika maongezi unavyowasiliana na watu wengine, na utakapojikuta unaongea na mtu kwa sauti kubwa na mtu huyo yupo karibu kiasi cha kuweza kumuongelesha kwa sauti ya chini na mkaelewana, itadhihirisha wazi kuwa kuna shida kati yako na Yule unayewasiana naye.
JITAHIDI KUEPUKA UGOMVI…. IMARISHA UPENDO …… PENDANA NA WATU….KUDUMISHA AMANI
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: NJIA RAHISI YA KUMTAMBUA MTU MGOMVI KWA NJIA YA KISAIKOLOJIA Description: Rating: 5 Reviewed By: mcjohnminja.blogspot.com
Scroll to Top