Habari Mpya

Saturday, January 09, 2016

ASILIMIA 80 YA WATU BARANI AFRIKA WANAUGUA UGONJWA WA SELIMUNDU

Imeripotiwa kuwa asilimia 80 wanatoka Barani Afrika, ambako Nigeria ni ya kwanza, ikifuatiwa na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na ya tatu ni Angola ikifuatiwa na Tanzania inashika nafasi ya nne kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa ambapo kila mwaka watoto 10,000 uzaliwa na siko seli. 

Akielezea kuhusiana na ugonjwa huu Mtaalam wa magonjwa ya watoto nchini Nairobi Aghakan Hospitali, Dr Wafulla Kennedy Charles alisema ugonjwa unahusu damu hasa kwa chembechembe hai kuganda na kuzuia damu kupita hivyo kusababisha mishipa kuziba na sehemu ambazo zinapokea damu kushindwa kupata hewa na chakula hali inayopelekea mgonjwa kuhisi maumivu

 Aidha Dr. Charles alisema Ugonjwa huu uanza kuonekana kutokana na chembechembe ndogo za damu kushindwa kufanya kazi, chanzo chake ni wazazi iwapo watakuwa na vinasaba vya siko seli na mtoto kuchukua vinasaba hivyo ndipo ugonjwa huo hutokea na hiyo huitwa siko seli anemia kurithi kutoka kwa wazazi.

Ni zipi dalili za ugonjwa wa siko seli?
Mara nyingi dalili za ugonjwa huu hutegemea na kiwango cha uathirikaji wa chembe chembe nyekundu za damu, miongoni wa dalili hizo ni upungufu wa chembechembe za damu mwilini, kizunguzungu pamoja na maumivu makali ya kichwa

 Naye Bi. Faudhia Juma Mkazi wa Manispaa ya Morogoro ni mama wa watoto ambao wana matatizo ya siko seli akitoa ushuhuda amesema ugonjwa huo umeanza kuonekana kwa watoto wake walipofika umri wa miezi tisa.

“Mwanzo ilikuwa ni ngumu kugundulika na kupatiwa tiba lakini baadaye ikagundulika kuwa ni siko seli hivyo watoto wangu wote wawili wana tatizo la siko seli tatizo ambalo walilipata kutokana na kurithi toka kwetu” alisema Bi Faudhia
 
Je ni madhara gani ambayo anaweza kupata mgonjwa wa siko seli?
Madhara ambayo mgonjwa anaweza kupata kutokana na ugonjwa wa siko seli ni kukabiliwa na maambukizi ya bakteria mwilini na Kiarusi.

Kwa upande wake Dr. Yusuph Almasi wa Idara ya Afya Mkoa wa Morogoro alibainisha kuwa ugonjwa huo ni wa kudumu hauna matibabu ya kuponya kabisa bali kinachofanyika wagonjwa wanapopata maumivu wanapewa dawa ya kutuliza maumivu hayo (Antpain)

Aliongeza kuwa wagonjwa hawa ni rahisi sana kupata magojwa tofauti kama Maralia, Nimonia na ni vema endapo anapata ugonjwa huu apewe tiba haraka kwa kuwa wagonjwa hawa hawana kinga yenye nguvu ya kupigana na magonjwa tofauti kama watu wengine

 “Ni kawaida kwa mgonjwa wa Siko Seli Anemia kupata upungufu wa damu hivyo wanalazimika kuongezewa damu ili kurudi katika hali ya kawaida na ikiwa damu inapungua kwa wingi wanatakiwa wapewe chanjo, chanjo hiyo ni muhimu sana kwa kila mtoto lakini kwa watu wa siko seli ni muhimu zaidi” alisema Dr.Almas.

Aidha Dr. Almas alisema imegundulika kuwa tatizo kubwa linalowakabili mara kwa mara wagonjwa wa Siko Seli ni nimonia, hivyo wagonjwa hao wanatakiwa kupata chanjo ya nimonia inayoitwa ‘nimokokobadseed’ kwa maana ya kuwapunguzia shambulio la ugonjwa huo

Unawezaje kupambana na ugonjwa wa siko seli?
Hata hivyo mwenyekiti wa mfuko wa Seli nchini Tanzania Grace Rubambey amesema hakuna tiba ya moja kwa moja mahsusi kwa ugonjwa wa siko seli hivyo matibabu hutofautiana kulingana na jinsi ugonjwa huo ulivyomuathiri mgonjwa, kuna wengine huongezewa damu, kuongezewa maji na hata wengine kupewa dawa za kutuliza maumivu.

Pia Rubambey amesema watoto wenye ugonjwa huu wanatakiwa wapewe chakula kilicho bora kutokana na magonjwa haya yanayowanyemelea mara kwa mara hiyo itasaidia kurudisha afya zao 

Ameongeza kuwa wakati mwingine wagonjwa hawa wanaweza kupata ugonjwa wa kupooza (strock) ambapo itawalazimu madaktari kuwaongezea damu kila mwezi mara moja ili kuzuia wasipate ugonjwa wa kukupooza (strock) kwa mara nyingine kwani wakipata ugonjwa huo kwa mara ya pili au ya tatu ni rahisi wakapoteza maisha yao.

Aidha wanandoa watarajiwa wanatakiwa kupima ugonjwa huu kabla hawajaamua kuzaa watoto ili kuepuka uwezekano wa kuzaa watoto wenye ugonjwa wa siko seli na kuwapa tabu katika maisha yao hivyo ni vema kuchukua hatua kwanza kwa kizazi kilicho salama.

Je nini sababu ya kukua kwa ugonjwa wa Siko Seli Tanzania?
Kwa upande wake Mratibu wa Kitengo cha Seli Mundu kutoka Hospital ya Taifa Muhimbili (MNH) Dr. Deogratius Soka amesema sababu kubwa inayofanya ongezeko kubwa la idadi ya watoto wenye ugonjwa wa siko seli ni kutokana na ufinyu wa uelewa kuhusiana na ugonjwa huo 

Pia amesema kuwa asilimia 15 ya watanzania wanavinasaba vya ugonjwa wa siko seli hivyo juhudi za makusudi zinatakiwa zifanyike kwa jamii kupatiwa elimu kuhusiana na ugonjwa huo.

Dr. Soka ameendelea kusema kuwa idadi kubwa ya wagonjwa  wa Siko Seli nchini wanapatikana katika Mikoa ya Tanga , Dar es Salaam, Pwani, Mara Mwanza, Bukoba, Shinyanga Tabora na Dodoma.

Kufikia hapa tumefikia tamati ya makala haya, hakika umeweza kuona ugonjwa wa Siko Seli maana yake na umeona jinsi unavyoambukizwa, pia tumeona njia ya kuweza kukabiliana nao japo kuwa hauponi, tukutane tena wiki ijayo katika Makala nyingine ya Afya.
kwa hisani ya Taty (Sua Media)
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: ASILIMIA 80 YA WATU BARANI AFRIKA WANAUGUA UGONJWA WA SELIMUNDU Description: Rating: 5 Reviewed By: mcjohnminja.blogspot.com
Scroll to Top