Good Morning.
Kwenye maisha kuna wakati utajikuta unalazimika kuanza upya baada ya kile ulichokuwa nacho kupotea ama ulichotarajia haujakipata.
Kwenye maisha kuna wakati utajikuta unalazimika kuanza upya baada ya kile ulichokuwa nacho kupotea ama ulichotarajia haujakipata.
Nimesoma habari za wengi na nimekutana na watu wengi sana
ambao walifanikiwa kuanza upya na kutimiza malengo yao baada ya kupitia
hali ngumu maishani mwao.Kuna mtu alipoteza familia yake yote Kwenye
ajali akabaki peke yake akaona kama vile maisha yamefika mwisho lakini
baada ya kuwa tayari kuanza upya na kukubaliana na yaliyotokea leo
ameweza kuyashinda maumivu yote na amefanikiwa kufikia ndoto yake.
Baada ya kushindwa kuendelea na shule na kujikuta akiishi
maisha ya mtaani baada ya wazazi wake kuachana akiwa na umri wa miaka 7
alikubali kuanza upya na leo Anthony Robins ana utajiri takribani dola
za kimarekani 400m,anamiliki ndege, majumba makubwa etc .
Baada ya kupitia mateso na uchungu wa kubakwa akiwa na
miaka 14 na kukataliwa mara nyingi alipoenda kutafuta Kazi za
utangazaji,Leo Oprah Winfrey sio tu anatangaza bali anamiliki vyombo vya
habari,ALIAMUA KUANZA UPYA.
Baada ya Steve Jobs kufukuzwa Kwenye kampuni ambayo
aliianzisha yeye mwenyewe,hakukata tamaa ya kutimiza ndoto yako.ALIAMUA
KUANZA UPYA.
Umefeli mtihani,umeachwa na umpendaye,biashara yako
imefilisika,umepoteza kila ulichonacho,umefukuzwa kazi...Usikubali kukaa
chini na kuanza kulia.AMUA KUANZA UPYA LEO.
Naona ndoto yako ikitimia, naona ukiwasaidia wengi
kufanikiwa kutokana na historia yako,naona ukiinuka na kuwainua wengi
watakaopitia hali kama uliyopitia.
Naamini Katika ndoto yako,
Naamini Katika Uwezo Wako,
Naamini Katika Hatima Yako.
By Joel Nanauka
See You At the Top.
Tembelea (www.JoelNanauka.Com) Ujifunze Zaidi
Tembelea (www.JoelNanauka.Com) Ujifunze Zaidi
0 comments:
Post a Comment