Habari Mpya

Tuesday, March 08, 2016

WAZAZI WAOMBA SEREKALI KUCHUNGUZA KWANINI WATOTO WAO WANAFELI SANA WILAYANI KARATU


WAZAZI wa vijiji vya Kata ya Barai iliyoko Wilayani Karatu Mkoani 
Arusha wameiomba Serikali ya awamu yaa tano kuchunguza sababu za watoto wao kufanya vibaya katika mitahani ya kuhitimu darasa la saba. 
 
Aidha alibainisha kuwa mbali na tatizo la umbali mrefu pia wanafunzi wamkuwa wakisumbuliwa na tatizo la njaa kwani shule hizo zimekuwa hasipikii wanafunzi mashuleni mchana kutokana na kutokuwa na bajeti hiyo.
 
Kwa upande wake mmoja wanafunzi hao ambao alijitambulisha kwa jina la Gilony Gitonyi alisema kuwa wamekuwa wanashindwa kusoma kutokana na njaa pamoja na kukosa mda wa kujisomea pindi wanaporudi nyumbani kwani muda mwingi wamekuwa wakiutumia kwa ajili kuchunga mifugo pindi wanaporudi majumbani.

Akizungumzia swala hilo mbunge wa jimbo la karatu Willy Qambalo alisema kuwa kwa upande wake anaona suluhisho la kutatua tatizo hilo ni pamoja na kujenga mabweni ilikuweza kuwasadia wanafunzi kupata elimu ili kila mwanafunzi asome apoapo shuleni ili kuweza kujipatia muda wa kujisomea. 

"unajua kujengwa kwa haya mabweni pia itasiadia kuwapata wanafunzi kirahisi ambao muda wamekuwa wakiacha masomo na kwenda kuchunga mifugo jambo ambalo linapingwa vikali na wazazi wa vijiji hivyo na pia wanafunzi hao watapata muda mrefu wa kujisomea na swala wao kupata njaa litapungua kwani kutakuwa na chakula shuleni kwa ajili yao"alisema Qakambalo

Aidha Tafiti zinaonyesha walimu ,wenye utovu wa nidhamu watoro na walevi katika maeneo ya mijini ndio hupelekwa katika shule hizzo zilizoko maeneo ya porini kama adhabu kwao.Swali la kujiuliza je mwalimu huyu atakuwa na nia ya kuwafundisha wanafunzi?Kupelekwa kwa mwalimu huyu kama adhabu badala ya eyey kuridhia Kujua kusomaa na kandika kwa wanafunzi hawa itakuwa ni ndoto.
Na Woinde Shizza,Karatu.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: WAZAZI WAOMBA SEREKALI KUCHUNGUZA KWANINI WATOTO WAO WANAFELI SANA WILAYANI KARATU Description: Rating: 5 Reviewed By: mcjohnminja.blogspot.com
Scroll to Top