Habari Mpya

Thursday, May 09, 2013

Hebu tupitishe macho na useme neno katika haya yalijiri nchini kwetu kwenye haya.....




Matokeo ya kidato cha 4 yalipotoka kati ya wanafunzi waliofeli kuna waliojiua. Kwa taarifa nilizonazo ni kuwa wanafunzi 4 waliripotiwa na vyombo vya habari kuwa walijiua! Pia kuna wale waliochanganyikiwa kisaikolojia ambao nadhani ni wengi sana japo hawajaripotiwa kwenye vyombo vya habari. 
Wiki iliyopita serikali ikasema kuwa kulifanyika makosa katika kupanga matokeo (grading) na ndio sababu KUBWA ya kufeli. Kwa hiyo re-grading and standardization inabidi vifanyike kwa kutumia mfumo uliotumika 2011 na sio mfumo mpya.

Sasa maswali yangu ni:-
1. Hao waliojiua matokeo yao yakirekebishwa na wakaonekana wamefaulu itakuwaje? Watafufuliwa ili waendelee na shule form 5 na 6?

2. Je kuna kitu kitafanyika kuwatibu wale waliopata matatizo ya kisaikolojia?

3. Je tuna uhakika gani kuwa mfumo uliotumika kupanga matokeo ni mpya na sio wa 2011? kama ni mpya ni sababu zipi zilipelekea kutumika kwa mfumo huo? Nani walioidhinisha? Na je katika kuruhusu matokeo yatangazwe ofisi husuka za serikali (Wizara ya Elimu, Baraza la mitihani na ile ofisi ya rais na waziri mkuu) zilliridhia matokeo yatangazwe? Na kama zilidhiria je ina maana kwa kukubali yarudiwe watakuwa wanakubali kula matapishi yao wenyewe?

4. Ni kwanini kumekuwa na ukimya mkubwa sana kutoka ofisi hizo tajwa hapo juu, mara tu baada ya kutoa tamko la kurudiwa?
Ni mawazo ya haraka haraka kichwani mwangu!!

according to Brother Chris
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: Hebu tupitishe macho na useme neno katika haya yalijiri nchini kwetu kwenye haya..... Description: Rating: 5 Reviewed By: mcjohnminja.blogspot.com
Scroll to Top