Habari Mpya

Saturday, August 24, 2013

MAPANGO YA AMBONI NI KIVUTIO KIZURI CHA ASILI



Wajaleo  waondoka  leo, ni msemo  wa watu wa mkoa wa Tanga, ila msemo  huu huendana  na mazingira yenyewe kutokana  na  ukarimu  waliokuwa nao  watu  waishio  mkoa  huo,  ama  kwa  hakika  ukisikia  mkoa   wa Tanga  utaamani  angalau  siku  mmoja   upotee  njia  ukajionee   mwenyewe,  kwani  mji  wa   Tanga  ni  mji  ambao  sio  mdogo  sana  wala  siyo mkubwa,  bali  ulijipatia  umaarufu   hivi  karibuni   kutokana  na  baadhi  ya  maeneo  kuwa   kama  sehemu  za vivutio  kwa  wageni  na  hata  wenyeji  waishio  nje  na  ndani  ya  mji  huo.


           Mkoa wa Tanga  umegawanyika  katika  Wilaya  saba  ambazo  ni  Handeni , Lushoto,  Kilindi, Korogwe,  Pangani,  Muheza  na  Tanga  yenyewe  bali  katika  wilaya  hizo  ni  Wilaya  ya  Tanga  ambayo  ndiyo  wilaya  iliyobeba  jumla ya wilaya zote  yenye vivutio vya kitakii  na  vya kiasili.

         Tukiangalia  katika  Wilaya  hii kunabadhi  ya  maeneo  yamekuwa  vivutio  vya  asili  kwa  wageni  na  hata kwa  baadhi  ya awatalii  wandani  ya mkoa  huo wa  Tanga,  kwani  mapango  ya  amboni  yamekuwa  kivutio kikuu cha  asili,  pia tukiangalia  hata  katika mbuga za wanyama  iliyoko  mkoani  humo  ambayo  inajulikana  kama  Sadani,  japo  leo nazungumzia  mapango  ya  asili  ya  amboni.

             
         Mapango  ya  amboni ni mapango ya asili kwa maana siyo ya mapango  yaliyo  tengenezwa  na  binadamu,  bali  mapango  haya  ni  matokeo  ya  mmomonyoko  wa  miamba ya chokaa ambayo  ni mabadiliko ya carboni na tukiangalia kwa  haraka tunaona  kuwa  kunamgawanjiko  wa  vitu kumi na tatu na kuanza  kuelezea  kimoja  baada  ya  kingine  na kueleza  kama  kinatumika au kilitumika vipi  hapo kale na hata sasa  kinatumikaje.

        Mapango haya yalianza shughuli  zake za utalii  mnamo  mwaka 1980 na 1990 kuanzia hapo wenyeji  wa mkoa huo walikuwa  wanatembelea mapango hayo bila ya malipo yoyote na  mnamo  mwaka 1999 ndipo walianza kufanya  malipo katika mapango haya kutokana  na baadhi  ya wenyeji  waishio karibu na mapango  hayo  kuanza  kutembelea  bila  utaratibu maalum  ndipo  walipoanza  utaratibu  wa  kulipia ili kuweka  mazingira  ya mapango  haya  katika hali ya usafi.

           Tukianza na kituo cha kwanza katika mapango haya ni kituo cha mzimu wa mababu ambao mnamo  karne ya 16 wananchi waishio katika mazingira hayo walitumia sehemu hiyo kufanyia ibada na matambiko katika sehemu hiyo na kwa sasa wanaitumia sehemu hiyo kama sehemu ya kufanyia matambiko hata kwa wageni wanaoingia nchini kwa lengo la kutalii na huitumia sehemu hiyo kama mmojawapo yakuomba kwa imani na kufanikiwa kwa walio wengi.

              Kundi lingine katika mapango hayo ni kituo ambacho hutumiwa kama maficho ya watu wawili ambao walipotea katika mapango hayo mmoja akiitwa Osale Otango na wa pili ni Paulo Hamisi hao watu walikuwa wanadaiwa kufanya fujo katika jamii na kuwapora wanaoingia ndani ya mapango na mara wafanyapo matukio hayo hukimbia katika mafichoyao, na watu hao waliishi zaidi ya miaka minne ndipo wanajamii walipo anza kuwatafuta na mbali yahayo yote watu hao bado wanakumbukwa kwa kile walicho kuwa wanakifanya katika mapango hayo mnamo mwaka 1950.

           Vilevile watu hao walikuwa wafanya yote hayo kutokana na taratibu ambazo waklikuwa hawakubaliani nazo ambazo walikuwa wafanyiwa na walowezi ndipo walipoamua kufanya fujo na kuwavamia walowezi hao.

             Hata hivyo kuna kunfi la nne ambalo simulizi zilidai kuwa mnamo mwaka 1941 wazungu waliingi na mbwa waliingia ndani ya mapango na kupotea japo hazikuishia hapo simulizi zilidai kuwa wazungu hao hawakutaka kuingia na mwenyeji na matokeo hao walipotea katika pango na pia inasemekana kuwa wenyeji wao walipofuatilia walikuta miguu ikielekea shimoni pia kwa simulizi hizi ziliendelea kuwa baada ya mwezi mmoja  na nusu mbwa alionekana katoka mlima Kilimanjaro na huo ndio mwisho wa simulizi hizi.

            Pia mapango hayo yamekuwa ni urithi wa Taifa na urithi wa utamaduni kwani hata kwa upande wa masomo kuna baadhi ya maeneo yamekuwa kama sehemu ya kujifunzia hasa katika somo la jiografia kuna baadhi ya miamba inakuwa na tabia kujiunga kama mvua ikinyesha miamba hiyo hutengeneza kitu kiitwacho stalactmait.

            Mbali na hayo tukiangalia mwisho wa Osale na Paulo umebaki kuwa historia kwani Paulo alifia Lushoto ambapo alimbaka mwanamke mnamo mwaka 1957 kwakuwa watu hao waliishi kwa miujiza na inasemekana kuwa mwnamke aliyebakwa na Paulo alipigwa risasi upande wakushoto na kuaga dunia.

            Hata kwa upande wa Osale naye alifariki mnamo mwaka 1958  huko na kwa mujibu wasimulizi hazikuelezwa alipofia na kama aliumwa au la,wote hao walizikwa huko Lushoto na huo ndio mwisho wa historia yao.Kwakusimuliwa huwezi kuamini jinsi ambavyo mapango hayo yalivyo kuwa kivutio kizuri kwa watilii wa nje ya nchi na hata kwa walio ndani ya nchi.tembelea mapango yetu yaliyo ndani ya nchi nzuri yenye amani na utulivu Tanzania.
                                                 






  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: MAPANGO YA AMBONI NI KIVUTIO KIZURI CHA ASILI Description: Rating: 5 Reviewed By: mcjohnminja.blogspot.com
Scroll to Top