Kuna aina
mbalimbali za mikate.Mara nyingi aina hutofautiana kutokana na viungo
vinavyotumika kutengenezea.
Katika mapishi leo
hii nitakuelekeza namna ya kutengeneza mkate wa ndizi.kama nilivyokueleza hapo
awali kwamba kuna tofauti kubwa baina ya mkate mmoja na mwingine.Jambo
linalosababishwa na kuwepo kwa viungo tofauti.
Mkate wa ndizi
umekuwa na tofauti kubwa ya ladha ukilinganisha na mikate mingine , hasa kwa
vile ina viungo tofauti na mikate ya kawaida.
Pamoja na kuwa aina
hii ya mikate imekuwa ukifahamika sana
katika maeneo yanayolima zao la ndizi.Bado imekuwa ni kazi kubwa kutengeneza.
Kwa kawaida vipimo
vya upishi huu hutegemea zaidi na idadi ya walaji ulionao.
Mahitaji
Sukari kikombe kimoja
Siagi theluthi kikombe
Mayai mawili
Maji theluthi kikombe
Unga wa ngano kikombe kimoja nanusu cha chai
Unga wa soda kijiko kimoja cha chai
Chumvi kijiko kimoja cha chai
Baking poda robo kijiko cha chai
Karanga nusu kikombe cha chai
Namna ya kupika
Changanya sukari na
siagi kwenye bakuli moja kubwa la udongo ama plastiki, hakikisha
vinachanganyika kabisa, kasha weak mayai na endelea kukoroga (hakikisha
unakoroga kwa kuzungusha upande mmoja tu), halafu weka unga wa ngano.
Vikishalainika weak
ndizi na saga kwa muda wa dakika tano. Ikiwa unatumia mashine ya kusagia
sekunde thelathini tu zinatosha.
Chukua viungo
vingine vyote vilivyobaki isipokuwa karanga na kasha weka kwenye mchanganyiko
wako. Changanya hadi vichanganyike vizuri na kasha waweza weka karanga endapo
utapenda.

Baada ya hapo ondoa
weka pembeni, acha upoe.Ukisha poa kabisa waweza kata mkate wako tayari kwa
kula.
Mkate huu unaweza
kula na chai ya maziwa ama kinywaji chochote kisichokuwa na kilevi.
Na; Maria Mtaita
0 comments:
Post a Comment