Habari Mpya

Friday, November 28, 2014

MFUKO WA PENSHENI WA LAPF NA HUDUMA YA HIFADHI YA JAMII KWA WOTE



www.lapf.or.tz

Mfuko wa Pensheni wa LAPF pamoja na kutekeleza majukumu yake ya kila siku kwa mafanikio makubwa, bado unafanya jitihada kubwa kuhakikisha kwamba huduma ya hifadhi ya jamii inamfikia kila mtu bila kujali aina ya ajira yake. Kwa mazingira ya sasa ya sekta ya Hifadhi ya Jamii, mtu yoyote mwenye shughuli za kuajiriwa au kujiajiri mwenyewe anaweza kujiunga na Mfuko wa LAPF katika utaratibu wa kisheria au wa hiari.

Kama wahenga wasemavyo maisha ni mipango, na hakuna aliyefanikiwa kimaisha na kudumu katika mafanikio bila ya kuwa na mipango madhubuti pamoja na njia za kutekeleza mipango hiyo iwe ya muda mfupi au mrefu.

Mfuko wa Pensheni LAPF ukiwa na dira ya “kuwa Mfuko bora wa Pensheni unaopendwa zaidi hapa nchini”, umeweza kubuni utaratibu unaomwezesha mtu yeyote kujiunga na kujiwekea akiba kwa lengo la kutimiza malengo mbalimbali ya maisha kupitia mpango wa LAPF-Uwekaji Akiba kwa Hiari au LAPF-Voluntary Savings Scheme (L-VSS). Kupitia mpango huu, mwanachama aliyejiunga anaruhusiwa kujiwekea akiba kulingana na kipato chake kwa wakati husika. Akiba inaweza kuwekwa kwa siku, wiki, mwezi au msimu kulingana na kipato cha mwanachama. Kiwango cha uwekaji akiba kinaweza kubadilika kulingana na hali halisi ya kipato.

Zifuatazo ni njia ambazo mwanachama anaweza kutumia kufikisha akiba LAPF; kupitia ofisi za LAPF zilizopo mikoa mbalimbali, benki (CRDB, NMB au NBC), Mitandao ya simu. Kila mwanachama awekapo akiba na kufika LAPF mwanachama hujulishwa na kuthibitishiwa kuhusu akiba yake. Pia kwa wanachama wenye uwezo wa kutumia mitandao wanaweza kuona akiba zao kupitia tovuti ya Mfuko www.lapf.or.tz
 
Walengwa wa mpango huu ni wale wote wenye uwezo wa kuzalisha kipato ikiwemo wakulima, wafanyabiashara, wavuvi, madereva teksi, bajaji, bodaboda n.k. Pia wale ambao wameajiriwa katika ajira rasmi na kuchangia kwenye Mifuko ya hifadhi ya jamii kwa utaratibu wa kisheria wanahamasishwa kujiunga na utaratibu huu ili kujiweka katika mazingira sahihi ya kustaafu kifahari.

LAPF inaamini mpango huu wa ni  kutimiza malengo na kujiwekea kinga yatokeapo majanga yanayopelekea kusitisha uzalishaji kwa muda au moja kwa moja kwani kwa atakayejiunga anaruhusiwa kuchukua mpaka asilimia 50, baada ya uwekaji wa akiba kwa kipindi cha mwaka mmoja na kuendelea ili kutatua changamoto mbalimbali ikiwepo kuboresha shughuli za kuzalisha kipato, pamoja na hayo pia mpango huu hauna makato ya aina yoyote kwa mwanachama zaidi ya kujipatia faida kila mwisho wa mwaka kutokana na mapato ya uwekezaji.

Uchangiaji wa hiari, unaweza kufanyika kwa namna mbili. Mfumo wa akiba na ule wa bima.
Mfumo wa akiba mwanachama anachangia kulingana na anavyopata na hivyo kustahili faida itokanayo na uwekezaji. Wakati wa mwisho hulipwa mkupuo unaohusisha michango na faida iliyopatika kutokana na mapato ya uwezaji kwa kipindi chote cha uanachama.

Mfumo wa bima kwa uchangiaji wa hiari hufanywa kwa mwanachama kuahidi kujiwekea kiwango maalum kisichopungua 20% ya kima cha chini cha mshahara wa serikali kwa kipindi chote. Mwanachama huyu akitimiza vigezo vya malipo ya uzeeni atalipwa kwa kanuni ya pensheni kama ilivyo kwa wachangiaji wa kisheria.

 Kwa mawasiliano zaidi;
E-mail:         info@lapf.or.tz
Cell phone: 0784-648085

“STAAFU KWA UFAHARI NA LAPF”
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: MFUKO WA PENSHENI WA LAPF NA HUDUMA YA HIFADHI YA JAMII KWA WOTE Description: Rating: 5 Reviewed By: mcjohnminja.blogspot.com
Scroll to Top