WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea misaada mbalimbali kwa ajili ya wakazi wa vijiji vya Mtondo na Nanjaru wilayani Ruangwa mkoani Lindi ambao nyumba zao ziliezuliwa na upepo Januari mwaka huu.
Akizungumza na wananchi wa vijiji hivyo (Jumapili, Februari 28, 2016), Waziri Mkuu alisema maafa huwa yanakuja bila kutarajiwa na akatumia fursa hiyo kuwashukuru wadau waliotoa misaada ya chakula, magodoro, mashuka, vitenge, mabati na mbegu za mazao.
Aliwataja wadau hao kuwa ni benki ya NMB, NSSF, wakazi wa Ruangwa na marafiki wa Ruangwa waishio Dar es Salaam ambao walifika kukabidhi misaada hiyo. 
Waziri Mkuu ambaye yuko kwenye ziara ya siku mbili katika mikoa ya Mtwara na Lindi  kukagua athari za mafuriko, hatua zinzochukuliwa za utoaji misaada kwa waathirika na kuwapa pole wananchi walioathirika na mafuriko hayo, alitumia fursa hiyo kuwataka wananchi waishio mabondeni wahame kwa sababu mvua kubwa bado zinakuja.
“Jambo hili si mipango ya mtu binafsi na sote tunajua kwamba tunahitaji mvua kwa ajili ya mazao lakini safari hii zimekuja zaidi ya kiwango cha kawaida. Mamlaka ya hali ya hewa imeshasema kuwa mvua kubwa zaidi zinakuja ifikapo Machi mwaka huu”, alisema.
Ili kuepusha maafa zaidi, kuanzia sasa, wale waliojenga mabondeni wanapaswa wahame. Pia nawasihi wananchi wachukue tahadhari wakiona mvua inakuja na upepo mkali wasikae ndani ya nyumba sababu hapa kijijini tumempoteza mzee wetu mmoja ambaye aliangukiwa na nyumba baada ya nyumba yake kuangukiwa na mti kutokana na mvua hizo,” aliongeza.
Kwa mujibu taarifa ya maafa iliyotolewa na Mkuu wa wilaya ya Ruangwa, Bi. Mariam Mtima, mvua zilizonyesha kati ya Januari na Februari mwaka huu zilisababisha nyumba 393 kuezuliwa na nyingine kubomoka na kuacha wakazi wa vijiji hivyo bila makazi.
“Zahanati ya kijiji cha Mtondo iliezuliwa paa, daraja la mto Muhuru limebomoka na halipitiki kabisa na ekari 1,186 za mashamba ya wananchi zimesombwa na maji. Mazao yaliyoathirika ni mahindi, muhogo, mikorosho, mtama, ufuta, kunde, mpunga na mbaazi,” alisema Mkuu huyo wa wilaya katika taarifa yake.
Alivitaja vijiji vingine ambavyo mafuriko hayo yaliharibu mashamba ya wananchi kuwa ni Nambilanje, Mkaranga, Namkatila, Chinongwe A, Likwachu, Nauname na Mbekenyera.
Alisema hali hiyo imesababisha upungufu mkubwa wa chakula wilayani humo na sasa hivi wanahitaji tani 1,133 za chakula aina wanga ambazo anataraji zitatosheleza mahitaji kwa mwezi Machi 2016.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU.MAJALIWAWaziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Nandagala wilayani Ruangwa ambao unafanywa kwa ufadhili wa kampuni ya HUAWEI ya China , kijijini hapo, Februari 28, 2016. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Jordan Lugimbana.
MAJALIWA3Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa ma  Mwanaidi Mussa  na Mkussa Lukoloma (kushoto) wote wa kijiji cha Nandagala wilayani  Ruangwabaada ya kuwakabidhi kadi zao za bima ya Afya ambazo zimegharimiwa na Kampuni ya Simu ya Halotel iliyochangia shilingi milioni tisa kuwawezesha wakazi wa kijiji hicho kufaidi huduma za Bima ya Afya.
MAJALIWA2Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea hundi ya shilingi milioni tisa kutoka kwa Mtalaam wa Ufundi wa Kampuni ya simu ya Halotel wa mkoa wa Lindi, Tran The Hoang ili ziweze kugharimia malipo ya kadi za bima ya Afya kwa baadhi ya wakazi wa kijiji cha Nandagala wilayani Ruangwa. Alikuwa katika ziara ya siku moja wilayani humo .
MAJALIWA4Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea msaada wa vyakula na nguo kutoka kwa Mwenyekiti  watu waliojitotelea kusaidia waliopatwa na maafa ya mvua katika kijiji cha Mtondo wilayani Ruangwa wakati Waziri Mkuu alipokwenda kijijini hapo kuwapa pole wananchi
MAJALIWA7Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wananchi wa Ruangwa baada ya kuwasili mjini hapo kwa ziara ya siku moja Februari 28, 2016. (Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu)



MUHIMU KWAKO....!!!
kama wewe ni mtafutaji wa kujitegemea au unatarajia kuja kuwa.... zingatia hii

JOINT SCOPE LTD imedhamiria kutoa msaada wa ushauri bure, kwa wanaotarajia au wanataka kusajili BUSINESS NAME au COMPANY LIMITED n.k.
 
hapa utaelezwa mchakato mzima na kila kinachohitajika wakati utakapotaka kufanya usajili wa kampuni au Jina la Biashara kupitia Brela, ambayo ndiyo mamlaka pekee Tanzania yenye mdhamana ya kusajili Kampuni (Company LTD) na Jina la Biashara (Business Name), Logo n.k.
 
Tumeamua kutoa huduma hii ya ushauri bure kutokana na kero za matapeli tulizokutana nazo na tulishindwa kuwatambua kutokana  na kutoweza watambua kwa kutojua ukweli halisi wa vinavyohitajika wakati wa usajili wa Kampuni ya JOINT SCOPE LTD.
 
"Ni vyema Kutafuta Elimu ya Jambo Unalotaka Kufanya Kwanza Kabla ya Kuanza Kufanya"

Kwa Mawasiliano
Simu: 0712 479 905

E-mail; jointscope@gmail.com

P.O. Box 2574 Morogoro - Tanzania

Huduma hii ni Bure kwa watanzania Tu!

ToGether We Can.....!!!!!