Habari Mpya

Thursday, March 03, 2016

Liverpool yaigeukia Man City, yaipiga goli 3 kwa bila

Baada ya mchezo wa fainali ya kombe la Carling na Manchester City kuibuka na ushindi dhidi ya Liverpool katika hatua ya penati timu hizo zimekutana tena usiku wa kuamkia Alhamisi katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza.

Mchezo huo ulimalizika kwa Liverpool kuibuka na ushindi wa goli tatu kwa bila, magoli ya Liverpool yakifungwa na Adam Lallana dakika ya 34, James Milner dakika ya 45 na Roberto Firmino katika dakika ya 57.

Baada ya ushindi huo, Liverpool imefikisha alama 41 na kushika nafasi ya 8 ya msimamo wa ligi ya Uingereza huku Manchester City ikisalia katka nafasi ya nne ikiwa na alama 47.

Matokeo ya michezo mingine iliyopigwa jana usiku ni;
Arsenal 1 – 2 Swansea City
Stoke City 1 – 0 Newcastle United
West Ham 1 – 0 Tottenham
Manchester United 1 – 0 Watford

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: Liverpool yaigeukia Man City, yaipiga goli 3 kwa bila Description: Rating: 5 Reviewed By: mcjohnminja.blogspot.com
Scroll to Top